Ambilikile Quotes

Quotes tagged as "ambilikile" Showing 1-2 of 2
Enock Maregesi
“Lakini kabla Rais hajaendelea kuongea, na ‘John Murphy wa Kolonia Santita’, Mogens aliruka na kumnyang’anya simu.
“Ambilikile,” Mogens aliita, akiangalia saa.
“Brodersen,” Sauti ya upande wa pili ilijibu, baada ya sekunde kumi.
“60111906,” Mogens alisema, baada ya sekunde kumi.
“57121906,” Sauti ya upande wa pili ikajibu, baada ya sekunde kumi.
“Jumapili,” Mogens aliendelea, baada ya sekunde kumi.
“Ijumaa,” Sauti ya upande wa pili ikajibu, baada ya sekunde kumi.
John Murphy wa Kolonia Santita aliposema ‘Ijumaa’, Mogens aliunda kicheko na kurusha mkono katika matundu ya kuongelea ya simu ...”
Enock Maregesi, Kolonia Santita

Enock Maregesi
“Ngumi ya Ambilikile ilitua barabara katika kichwa cha Brookshield na kuleta madhara makubwa. Sehemu moja ya kichwa, cha Brookshield, ilibonyea kabisa! Kimya kilichotawala kiliwasisimua mashabiki. Walipovamia ulingo, kushuhudia kisichoweza kufikirika, walitoka pale wakiwa na hakika ya asilimia 100; kwamba John alikuwa na nyundo (au chuma chochote) katika mfuko wake wa bukta – aliyoitoa (harakaharaka), wakidhani ni mtindo wa kipigo, na kumpondea mwenzake kichwani! Ile haikuwa nyundo. Wala haukuwa uchawi. Ilikuwa ngumi, imara, ya uzito wa kilo 90; uzito wote wa John Ambilikile.”
Enock Maregesi, Kolonia Santita