“Kiswahili ni lugha ya Kibantu na lugha kuu ya kimataifa ya biashara ya Afrika ya Mashariki ambayo; maneno yake mengi yamepokewa kutoka katika lugha za Kiarabu, Kireno, Kiingereza, Kihindi, Kijerumani na Kifaransa, kutoka kwa wakoloni waliyoitawala pwani ya Afrika ya Mashariki katika kipindi cha karne tano zilizopita.
Lugha ya Kiswahili ilitokana na lugha za Kisabaki za Afrika Mashariki; ambazo nazo zilitokana na Lugha za Kibantu za Pwani ya Kaskazini Mashariki za Tanzania na Kenya, zilizotokana na lugha zaidi ya 500 za Kibantu za Afrika ya Kusini na Kati.
Lugha za Kibantu zilitokana na lugha za Kibantoidi, ambazo ni lugha zenye asili ya Kibantu za kusini mwa eneo la Wabantu, zilizotokana na jamii ya lugha za Kikongo na Kibenue – tawi kubwa kuliko yote ya familia ya lugha za Kikongo na Kinijeri katika bara la Afrika. Familia ya lugha za Kikongo na Kibenue ilitokana na jamii ya lugha za Kiatlantiki na Kikongo; zilizotokana na familia ya lugha za Kikongo na Kinijeri, ambayo ni familia kubwa ya lugha kuliko zote duniani kwa maana ya lugha za kikabila.
Familia ya lugha ya Kiswahili imekuwepo kwa karne nyingi. Tujifunze kuzipenda na kuzitetea lugha zetu kwa faida ya vizazi vijavyo.”
―
Lugha ya Kiswahili ilitokana na lugha za Kisabaki za Afrika Mashariki; ambazo nazo zilitokana na Lugha za Kibantu za Pwani ya Kaskazini Mashariki za Tanzania na Kenya, zilizotokana na lugha zaidi ya 500 za Kibantu za Afrika ya Kusini na Kati.
Lugha za Kibantu zilitokana na lugha za Kibantoidi, ambazo ni lugha zenye asili ya Kibantu za kusini mwa eneo la Wabantu, zilizotokana na jamii ya lugha za Kikongo na Kibenue – tawi kubwa kuliko yote ya familia ya lugha za Kikongo na Kinijeri katika bara la Afrika. Familia ya lugha za Kikongo na Kibenue ilitokana na jamii ya lugha za Kiatlantiki na Kikongo; zilizotokana na familia ya lugha za Kikongo na Kinijeri, ambayo ni familia kubwa ya lugha kuliko zote duniani kwa maana ya lugha za kikabila.
Familia ya lugha ya Kiswahili imekuwepo kwa karne nyingi. Tujifunze kuzipenda na kuzitetea lugha zetu kwa faida ya vizazi vijavyo.”
―
“Sanjay Kanaka Ramachandra, 'The Satellite', baada ya kutoka Korea ya Kaskazini na Salina Cruz kwa ajili ya kozi maalumu ya ugaidi na kwa ajili ya Kiapo cha Swastika kwa mpangilio huo, alirudi Mumbai kusimamia shughuli za Kolonia Santita za bara la Asia na Australia – kwa uaminifu wa Sheria ya Kitalifa ya Kolonia Santita. Ramachandra, anayeitwa 'The Satellite' kwa sababu ya jina lake la mwisho, alipewa pia jukumu la kuyachunga Makao Makuu ya Kanda ya Asia-Australia ya Tume ya Dunia; na kupeleka taarifa yoyote ya kijasusi (inayohusiana na WODEC-Rangoon) Mexico City kwa ajili ya maamuzi ya Mkurugenzi wa Usalama wa Kolonia Santita Gortari Manuel. Mojawapo ya operesheni kubwa alizowahi kuzifanya Ramachandra kwa niaba ya Kolonia Santita ni kuingiza nchini India mzigo wa tani 350 za majani ya koka, ijapokuwa tani 37 zilikamatwa na mamlaka za kuzuia madawa ya kulevya za India na za Tume ya Dunia, na kusambaza kilo 560 za kokeini safi (isiyokuwa na doa) katika nchi zote za Asia na Australia ndani ya siku 14.”
―
―
“Ukiua mtu bila kumwambia kwa nini unamuua anaweza kujua umemuua kwa kumwonea. Akijua umemuua kwa kumwonea roho yake inaweza kukusumbua wewe na familia yako maisha yenu yote. Makachero wa EAC wana leseni ya kuua. Lakini si kuua ovyo kama James Bond. Kila wanayemuua lazima waandike ripoti kwa nini wamemuua. Kachero wa EAC akiua mtu, kwa makosa, kwa bahati mbaya, atalindwa na Mwenyezi Mungu. Atalindwa na Tambiko la Tume ya Dunia.”
―
―
Goodreads Librarians Group
— 320567 members
— last activity 1 minute ago
Goodreads Librarians are volunteers who help ensure the accuracy of information about books and authors in the Goodreads' catalog. The Goodreads Libra ...more
Leanne’s 2025 Year in Books
Take a look at Leanne’s Year in Books, including some fun facts about their reading.
More friends…
Favorite Genres
Polls voted on by Leanne
Lists liked by Leanne






















