,

Mataifa Quotes

Quotes tagged as "mataifa" Showing 1-5 of 5
Enock Maregesi
“Sabato ilianzishwa na Mungu siku ya saba ya uumbaji wake. Siku ya Sabato ni siku takatifu, iliyoko katika Amri Kumi za Mungu, ambayo hatuna budi kuitunza na kuiheshimu. Sheria ya Siku ya Sabato haikufa baada ya kifo cha Yesu Kristo msalabani kama Wakolosai wanavyodai. Wakolosai walifuata falsafa za kipagani, na walizileta falsafa hizo ndani ya mwili wa Kristo ambalo ni kanisa. ‘Usiiamini’ Wakolosai 2:17. Iamini Wakolosai 2:20-23, ambapo Paulo anafundisha Mataifa jinsi ya kuitunza Sabato, na 1 Wakorintho 12:27 ambayo inatoa maana halisi ya Wakolosai 2:17. ‘Mwili wako ni wa Kristo’ ni tofauti na ‘mwili wa Kristo’ na ni tofauti na kanisa. Ukiamini kama mwili wako ni wa Kristo na ni kanisa, utaitunza Sabato.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu alitengeneza familia. Alitengeneza koo, makabila na mataifa, ili watu wajuane na kuheshimiana.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kama George Bush angekuwa na amani ndani ya moyo wake na Saddam Hussein angekuwa na amani ndani ya moyo wake Vita ya Ghuba isingetokea. Vilevile, katika kitabu cha ‘Kolonia Santita’, kama Rais wa Tume ya Dunia angekuwa na amani ndani ya moyo wake na kiongozi wa Kolonia Santita angekuwa na amani ndani ya moyo wake Kolonia Santita isingepigana na Umoja wa Mataifa. Taifa lisingepigana na taifa, na mataifa yasingepigana na magaidi.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Sababu ya kupanda na kuanguka kwa mataifa ni ya kimaadili na kiroho. Hakuna taifa linaloweza kutegemea nguvu na mali zake ili kujiokoa kutokana na madhara ya ukiukwaji wa maadili.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Taifa ni mataifa. Ukitambuliwa na taifa utatambulika kimataifa.”
Enock Maregesi