Taifa Quotes

Quotes tagged as "taifa" Showing 1-9 of 9
Enock Maregesi
“Mungu alilibariki taifa la Israeli katika misingi ya kidini na si katika misingi ya kisiasa au misingi ya kihistoria; na asili ya dini ya Kikristo ni kutoka katika taifa hilo ambalo Biblia imelitaja kama taifa teule la Mwenyezi Mungu. Mgogoro wa Israeli na Palestina ulianzishwa na Israeli mwenyewe. Yakobo alipokea baraka iliyokuwa si ya kwake kwa kutumia hila ya Rebeka. Baraka ya Yakobo ilikuwa ya Esau.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kama George Bush angekuwa na amani ndani ya moyo wake na Saddam Hussein angekuwa na amani ndani ya moyo wake Vita ya Ghuba isingetokea. Vilevile, katika kitabu cha ‘Kolonia Santita’, kama Rais wa Tume ya Dunia angekuwa na amani ndani ya moyo wake na kiongozi wa Kolonia Santita angekuwa na amani ndani ya moyo wake Kolonia Santita isingepigana na Umoja wa Mataifa. Taifa lisingepigana na taifa, na mataifa yasingepigana na magaidi.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Sababu ya kupanda na kuanguka kwa mataifa ni ya kimaadili na kiroho. Hakuna taifa linaloweza kutegemea nguvu na mali zake ili kujiokoa kutokana na madhara ya ukiukwaji wa maadili.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Dhambi ikizidi katika taifa, Mungu ataliangamiza. Taifa likitenda haki, Mungu ataliinua.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Uovu ni aibu kwa taifa zima!”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Wakati Yuda ikiongozwa na kiongozi mzuri na mwenye haki kama Yosia, taifa lilistawi. Lakini ilipokuwa chini ya mwovu Manase, taifa lilisambaratika. Katika karne hii, Uingereza ilipata msukosuko mkubwa mwaka 1936 juu ya uamuzi wa Edward VIII kuoa mwanamke wa Kimarekani aliyekuwa mtalaka Wallis Simpson. Uamuzi huo ulisababisha matatizo makubwa ya kikatiba, na nusura serikali ya Uingereza ijiuzuru. Hata hivyo, kaka yake mdogo, George VI, kwa mapenzi makubwa na nchi yake, huku akikataa katakata kuondoka London wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia, aliliongoza taifa hilo katika kipindi kigumu zaidi kuliko vyote katika historia ya Uingereza. Kanuni hii ya uongozi ina ukweli katika jambo lolote kubwa na hata dogo la ujasiri.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Taifa ni mataifa. Ukitambuliwa na taifa utatambulika kimataifa.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Taifa ni malaika! Taifa ni Shetani! Laana ya mwenye haki ina haki.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Fidel Castro alitenda haki katika taifa lake ndiyo maana Mungu akamsaidia yeye na wananchi wake. Ijapokuwa ameondoka, lakini fikira zake sahihi zitaendelea kuwepo. Taifa la Kuba Mungu ataendelea kulibariki, kwa sababu fikira za Wakuba ni fikira za Fidel Castro.”
Enock Maregesi